• Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe za watumishi |
    • Malalamiko |
Kyerwa District Council
Kyerwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa

  • Mwanzo
  • kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Teknolojia, Habari na Mawasiliano
      • Ufugaji wa Nyuki
    • Kata
      • Kata zetu
  • Fursa za uwekezaji
    • Kivutio cha Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Viwanda
  • huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Elimu, Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
    • Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Wateja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Maktaba ya picha
    • Huotuba za Viongozi
    • Video

Mifugo na Uvuvi

Mifugo na Uvuvi ni shughuli inayofanywa na wakazi wengi wa Wilaya ya kyerwa. Halmashauri kupitia Idara ya Mifugo na uvuvi imekuwa na mikakati thabiti ya kuhakikisha sekta hii inakuwa na matokeo chanya ya kuwainua kiuchumi Wavuvi na wafugaji waliotapakaa karibu Wilaya yote ya Kyerwa.

Kwa kuzingatia hili Halmashauri imeandaa andiko la mradi wa uwekezaji "District Investment Profile" katika sekta hii ambapo wawekezaji wanaweza kuja kuwekeza katika kuboresha thamani ya mazao yatokanayo na Mifugo na Uvuvi.

Miundombinu ya Mifugo iliyopo Wilayani

Majosho: Halmashauri ina jumla ya majosho 8 katika Kata za Mabira, Kimuli, Murongo, Bugomora, Isingiro (mawili ambayo ni Siina, na Kanyina), na Nkwenda. Majosho haya yote yanahitaji ukarabati ili yaweze utumika kwa kuwa yana ubovu wa viwango tofauti.

Malambo: Halmashauri ina lambo moja tu la Kyerwa ambalo lilichimbwa na wananchi kwa nguvu yao. Lambo hili limejengwa katika Kijiji cha Kyerwa kupitia njia shirikishi ya Fursa na Vikwazo kwa maendeleo (O & OD) iliibua mradi huu. Hata hivyo mradi huu umebadilishwa baada ya sehemu iliyokuwa imepangwa kwa shughuli hiyo kutengwa kwa ajili ya ujenzi wa Makao Mkuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa.

Machinjio: Kwa sasa Wilaya haina machinjio kubwa na ya kisasa, bali kuna sehemu tano (Machinjio ndogo) za watu binafsi ambazo zinatumika kwa ajili ya uchinjaji (miamba). Hata hivyo halmashauri imekwisha ainisha eneo la Rubwera kwa wawekezaji kuja kuwekeza katika Ujenzi wa Machinjio ya kisasa.

Minada ya Mifugo: Kuna mnada mmoja wa awali katika kijiji ya Katera.Hata hivyo shughuli za biashara ya mnada wa mifugo zimefungwa kutokana na kuwepo kwa karantini yamlipuko wa ugonjwa wa Miguu na midomo (F.M.D) katika wilaya ya Kyerwa.

Vibanio: Kuna vibanio vitatu katika maeneo ya Businde, Katera, na Ruhita. Vibanio hivyo hutumika katika kuwadhibiti Ng'ombe wakati wa kutoa huduma mbalimbali za Mifugo kama vile chanjo, kukata pembe na n.k.

Magonjwa ya Mifugo

Magonjwa ya mifugo yanayoathiri mifugo katika Wilaya ya Kyerwa ni yale yaenezwayo na Kupe kama vile Ndigana kali, Ndigana baridi, na moyo maji. Vilevile kuna magonjwa yaenezwayo na Mbung'o kama vile ugonjwa wa miguu na midomo, pamoja na BQ. Dalili za ugonjwa wa mapafu ya ng'ombe (C.B.P.P) zimeonekana katika kata ya Kaisho na Isingiro.

Ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa miguu na midomo tarehe 27 Julai 2012 iliwekwa karantini dhidi ya ugonjwa wa miguu na midomo. Eneo lote la Wilaya ya Kyerwa limeathirika.

Chanjo ya kuzuia Magonjwa ya Mifugo

Katika suala zima la kuzuia na kujikinga na magonjwa ya Mifugo, Chanjo mbalimbali za mifugo hutolewa na idara ya Mifugo na Uvuvi.

Pamoja na kuweka karantini, jitihada za kuzuia kuenea kwa maambukizi mapya ya ugonjwa wa miguu na midomo zinafanyika kwa kuwahamasisha wafugaji kuchanja Ng'ombe wao.

Uhimilishaji wa Mifugo

Hakuna shughuli za uhamilishaji zinazofanyika.Wafugaji wanahamasishwa ili kuibua mradi wa uhimilishaji wa mifugo ili kuboresha mifugo yao haraka na kuongeza tija na uzalishaji wa mifugo na mazao yake. Kwa kupitia mpango wa kilimo wa Wilaya (DADPs) uwezeshwaji utafanyika baada ya mpango huo kuibuliwa na wanufaika.Aidha, Wafugaji wanahamasishwa kuunda vikundi watakavyotumia kuchangia gharama kumpeleka kijana ambaye atagharamiwa ili kupata mafunzo juu ya uhimilishaji ili baadaye aje kutoa huduma hiyo kwenye maeneo ya wafugaji.

Uvuvi

Uvuvi ni mojawapo ya shughuli muhimu hapa Wilayani kwa kuwa yapo maziwa madogo yapatayo 7 na zipo jitihada za kuchimba malambo 4 ya kufugia samaki na kuzalisha vifaranga vya samaki.

Shughuli za uvunaji wa mazao ya Uvuvi Wilaya ya Kyerwa zinafanyika katika Maziwa madogo (Sattelite Lakes), Mabwawa na Mto Kagera , Samaki wanaopatikana ni Sato (Tilapia), Kambare (Catfish), na Kamongo (Lung fish).


Taarifa ya mwaka ya Maendeleo ya Mifugo na Uuvi bonyeza TAARIFA YA MWAKA MIFUGO.pdf kusoma zaidi

Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KYERWA December 14, 2022
  • Kuitwa kwenye usahili nafasi za Udereva Daraja la II utakaofanyika kuanzia tarehe 20/11/2022 mpaka tarehe 21/11/2022 November 14, 2022
  • Tangazo la Nafasi ya Udereva TGS B Nafasi 02 -Limerudiwa Mwisho tarehe 18/08/2022 August 11, 2022
  • Mlipuko wa ugonjwa wa kichaa cha Mbwa May 17, 2018
  • Tazama vyote

Habari mpya

  • Bilioni 1.2 zajenga vituo 2, na Zahanati 2 Kyerwa

    January 09, 2023
  • Ujio wa Mwenge wa Uhuru Wilayani Kyerwa

    October 06, 2022
  • "Hatutalala,hatutapumzika kuhakikisha ugonjwa wa Ebola hauingii Nchini " Waziri Ummy Mwalimu

    October 05, 2022
  • Mkurugenzi akerwa na uvamizi wa maeneo ya vituo vya wakulima

    September 26, 2022
  • Tazama vyote

Video

Kamati ya siasa ukaguzi wa Miradi Kyerwa
Video zaidi

Viungio

  • Dira na dhima ya Halmashauri
  • Maktaba ya picha

Viungio linganishi

  • Tovuti ya Mkoa wa Kagera
  • Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa
  • Salary Slip
  • Ofisi ya Rais, TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
  • Ikulu

Kifuatilia wageni

world map hits counter

Mapokezi ya wageni

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    Kyerwa District Council

    Anuani ya Posta: P.O Box 72, KYERWA

    Simu ya mezani: +255 686 397 972

    Simu ya Mkononi: +255 754 422 746

    Barua pepe : ded@kyerwadc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki©2017 GWF, Kyerwa District Council. All Rights Reserved